HeCo Poultry Farm

HeCo Poultry Farm we are selling Agricultural products like chickens and also we provide agricultural eduction

19/04/2022

MAKOSA MATANO WANAYOFANYA WAFUGAJI.

Wafugaji wengi huwa na kasumba au matatizo mengi katika kuendesha biashara zao za ufugaji ikiwemo na:

1. Kujua undani wa mbegu anayoingiza shambani kwake.
Hili ni tatizo linalosumbua wafugaji wengi na kwa muda mrefu sasa, yaani mfugaji akisikia kuna mtu anauza KUCHI na yeye atataka bila kujua ni mbegu gani ya kuchi, ubora wao upoje na udhaifu wao upoje ila kwa kuwa kaambiwa kuchi wanalipa utakuta anakimbizana kuingiza hiyo mbegu shambani bila kukusanya taarifa sahihi kwa lengo la kuokoa mtaji wake na malengo yake.

2. Kutokuwa na mtaalamu wa kuaminika.
Wafugaji wengi hawana wataalamu wa uhakika yaani huwa na madaktari wengi kiasi kwamba ikitokea mifugo yake inaumwa huwa anachanganya madawa hadi mfugo unachanganyikiwa.

3. Malengo makubwa ya ufugaji wake.
Wafugaji wengi huwa hawana malengo endelevu ya ufugaji hali hii huwafanya wawe ni watu wasio na misimamo ya bei na ubora unaoeleweka.
Ni miaka sasa kuku wa nyama wanauzwa 5000+ na hata k**a vifaranga vitauzwa bei basi ukosefu wa misimamo hujikuta wajasiriamali wengi wafugao kuku huishia kulalamika na sio kusimamia wanachokiamini.

4. Elimu ya ujasiriamali na uwekezaji
Ni tatizo linalowafanya wafugaji wabaki palepale licha ya kuwa na mitaji ila ukosefu wa elimu umesababisha mitaji kufa na masoko kudumaa miaka yote.

5. Muendelezo
Ni hatua ya kuendeleza kile ulichokianza, hii imesababishwa na tabia ya mazoea iliyopelekea wateja hao wakose biashara endelevu.

baadaye

28/03/2021
11/08/2020

Habari zenu nyote.
naomba muwe makini katika kipindi hiki ambacho hatutoi huduma yoyote iwe ni kuuza vifaranga,kuku wakubwa wala mayai na huduma zote za ufugaji.
kutokana na hilo napenda kuwakumbusha wale ambao wanatudai tunaelewa uvumilivu wenu na ustaarabu nasi tutajitahidi kwa kadri tuwezavyo tuwamalize nyote na kuendelea na majukumu yetu k**a kawaida.

HABARIKwa sasa hatutoi huduma wala uzalishaji wa aina yoyote ile ya kuku.Tupo kwenye kipindi cha kulipa wadeni wetu hivy...
06/04/2020

HABARI
Kwa sasa hatutoi huduma wala uzalishaji wa aina yoyote ile ya kuku.

Tupo kwenye kipindi cha kulipa wadeni wetu hivyo tunaomba mtuvumilie katika kipindi hiki kigumu kwetu na kwenu pia.

Tutakaporejea tutawajulisha.

TANGAZO   TANGAZOOTunapenda kuwataarifu kuwa kuna changamoto ya kiuzalishaji iliyotupata kwa majuma manne sasa hali iliy...
17/09/2018

TANGAZO TANGAZOO

Tunapenda kuwataarifu kuwa kuna changamoto ya kiuzalishaji iliyotupata kwa majuma manne sasa hali iliyopelekea kuwe na foleni ya watu ila kuanzia leo tar 17-21/09/2018 tutakuwa tumemaliza foleni yote na tutaendelea na oda za mbele k**a kawaida.

mtuwie radhi kwa usumbufu uliojitokeza.
pia tunapenda kuwataarifu wateja wote tuliokuwa tunawakopesha vifaranga kuwa TUMEFUNGA ZOEZI LA KUKOPESHA VIFARANGA KUTOKANA NA TATIZO LILOTUPATA KWENYE UZALISHAJI HADI HALI ITAKAPOTENGEMAA MWISHONI MWA WIKI HII.

Imetolewa na idara ya mawasiliano na habari HeCo Poultry.

JE, WAJUA??Vifaranga wengi huwfa kwa wafugaji bila kujua tatizo la vifo hivyo.wafugaji wapya na wale wenyeji hukutana na...
22/08/2018

JE, WAJUA??

Vifaranga wengi huwfa kwa wafugaji bila kujua tatizo la vifo hivyo.

wafugaji wapya na wale wenyeji hukutana na changamoto ya vifo pindi waingizapo vifaranga bandani hali inayopelekea wakate tamaa ya ufugaji.

leo tunapenda kukupa hints hizi ili kuzuia vifo mfululizo bandani kwako.

=> hizi ni dondoo zinazoweza kukusaidia kunusuru vifo katika ufugaji wako wa kuku na jamii yoyote ile ya mifugo.

1. Joto
ni lazima liandaliwe masaa mawili au matatu kabla haujaingiza vifaranga bandani.
* hakikisha joto lako linaendana na umri wa vifaranga vyako.
* hakikisha unatumia vyanzo vizuri vya joto ili kuzuia vifaranga visipate madhara katika mapafu au mfumo wao wa hewa.

MKAA
Hakikisha unawasha mkaa wako nje ya banda na umekolea wote, usiwashe mkaa ndani ya banda au kuongezea mkaa kwenye moto unaoelekea kuisha ukiwa bandani bali toa nje kisha uongezee na kuukoleza hadi uwake wote.
Hii ni kutokana na mkaa kuwa na sumu ya carbon monoxide hewa hii huwa na madhara kwa binadamu na hata viumbe vingine vyenye uhai k**a mifugo n.k
Sumu hii ikiingia katika mfumo wa hewa wa kuku au kifaranga huanza kumdhoofisha taratibu na hupelekea kifo au vifo vingi kwa wakati mmoja.

2. Hali ya Banda
weka banda katika hali ya usafi na kavu.
wafugaji wengi hujisahau katika kulea vifaranga na kuzingatia kanuni bora za ufugaji vifaranga, utakuta ndani ya banda kumemwagwa mwagwa maji hali inayopelekea kuwe na unyevunyevu au hata kupelekea uvundo na hii husababisha vifo kwa vifaranga wa siku moja au hata wiki au wiki 2 ( Jitahidi sana kukinga kuliko kutibu maana unaweza ukatafuta tiba na ukaikosa vile vile.)

Kwa haya na mengine mengi tuzidi kuwa pamoja mahali hapa, nasi tutakupa mbinu mbalimbali za kufikia ufugaji bora na wa wenye tija.

By HeCo Poultry Farm

itaendelea......................

hatimaye tulifika Mvuti.hakika HeCo Poultry Farm tunapokelewa vizuri sana.nasi hatutawaangusha wateja wetu
18/08/2018

hatimaye tulifika Mvuti.
hakika HeCo Poultry Farm tunapokelewa vizuri sana.

nasi hatutawaangusha wateja wetu

Safari ya kusambaza vifaranga vya Broiler kwenda kwa wateja ikiwa imefika kwa mteja wetu maeneo ya Kisukuru - Reef Garde...
18/08/2018

Safari ya kusambaza vifaranga vya Broiler kwenda kwa wateja ikiwa imefika kwa mteja wetu maeneo ya Kisukuru - Reef Garden.
Asanteni nyote mnaotuamini na kufanya biashara na sisi www.Facebook.com/HeCoPoultryFarm

tupo tayari kufanya kazi na wengi zaidi,
Bei ya vifaranga ni:

Broiler 1600/=

Malawi/Australorp
Day 1 ni Tshs. 1500/=
week ni 2300/=
Mwezi ni 4000/=

Kuroiler
Day 1 ni 2000/=
week ni 2500/=
mwezi ni 5000/=

Sasso
Day 1 ni Tshs. 1800/=
week ni 2400/=
mwezi ni 4500/=

Kienyeji pure
Day 1 ni 2000/=
week ni 2500/=
mwezi ni 5000/=

wasiliana nasi kwa
0754927820
0764340878

Tupo Ukonga, Dar Es Salaam

karibuni sana

17/08/2018
15/08/2018
Hawa wametimiza wiki 2 sasa yaani tarehe 15/08/2018 wametimiza wiki 2.hadi wiki ijayo wataanza kuhesabiwa masaa ya kuing...
15/08/2018

Hawa wametimiza wiki 2 sasa yaani tarehe 15/08/2018 wametimiza wiki 2.

hadi wiki ijayo wataanza kuhesabiwa masaa ya kuingizwa sokoni.
Tumekubali kuwa Fahari ya wafugaji.

wengi wanazidi kuweka oda,Sisi ni fahari yako ewe mfugaji
13/08/2018

wengi wanazidi kuweka oda,
Sisi ni fahari yako ewe mfugaji

Moja ya wateja wetu waliopokea vifaranga Alhamisi hii, Chanika,Dar Es Salaam
12/08/2018

Moja ya wateja wetu waliopokea vifaranga Alhamisi hii,
Chanika,Dar Es Salaam

Tunamshukuru Mungu tumevuna salama mpunga na sasa tunasubiria mwezi wa 10 na 11 tuuingize Dar kwa ajili ya biashara.HeCo...
11/08/2018

Tunamshukuru Mungu tumevuna salama mpunga na sasa tunasubiria mwezi wa 10 na 11 tuuingize Dar kwa ajili ya biashara.

HeCo Farm ni zaidi ya ufugaji.
KURIDHIKA KWAKO NDIYO SIFA YETU (HeCo Multi Services)

04/08/2018
Hatimaye tukaenda Pugu hii sasa tukaiita TWENDE BANDANI CAMPAIGN.tumekuta mengi katika mabanda ya wafugaji, hii imesaidi...
03/08/2018

Hatimaye tukaenda Pugu hii sasa tukaiita TWENDE BANDANI CAMPAIGN.

tumekuta mengi katika mabanda ya wafugaji, hii imesaidia kuwashauri na pia kujifunza uzoefu wao kuhusu field hii ya ufugaji.
usihofu tutakufikishia vifaranga hadi bandani kwako.
fuatilia video clip zinazofuata kwa maelezo zaidi kuhusu kuku wetu na ukuaji wao.

ukitupa nafasi nasi tunaitendea haki kwa kukufikishia vifaranga vyako hadi shambani mwako.huyu ni mteja wetu wa Kibaha S...
03/08/2018

ukitupa nafasi nasi tunaitendea haki kwa kukufikishia vifaranga vyako hadi shambani mwako.
huyu ni mteja wetu wa Kibaha Sheli mkabala na mizani ya zamani, aliweka oda ya vifaranga na jana tar 2/08/2018 tumemfikishia oda yake vifaranga 400.

ni ndani ya wiki tatu tu unapata oda yako.

Dada Rehema hongera kwa kazi nzuri na songa mbele, changamoto zitokeapo simama songa mbele.mazingira mazuri hufanya kazi...
26/07/2018

Dada Rehema hongera kwa kazi nzuri na songa mbele, changamoto zitokeapo simama songa mbele.

mazingira mazuri hufanya kazi izidi kuwa nzuri, usirudi nyuma bali jiboreshe

have you come across with these Terminologies?Learn with us.
18/07/2018

have you come across with these Terminologies?

Learn with us.

Layers wanaotaga.Karibu tufuge.
11/07/2018

Layers wanaotaga.

Karibu tufuge.

Incubation Process for birds eggs.(mtiririko wa kuangulisha mayai ya ndege k**a kuku,bata n.k)
04/07/2018

Incubation Process for birds eggs.
(mtiririko wa kuangulisha mayai ya ndege k**a kuku,bata n.k)

Maendeleo ya yai hadi kufikia kuanguliwa
03/07/2018

Maendeleo ya yai hadi kufikia kuanguliwa

01/07/2018

Ufugaji ni mahesabu na ufugaji ni vipimo bila vipimo hauwezi pata namba kamili.
upate wapi vifaranga,
uleaje,
ushike vipi soko n.k
ni moja ya vitu vya msingi katika ufugaji na ndio hukupa vipimo na mahesabu ya ufugaji wako.

www.facebook.com/HeCoPoultryFarm

26/06/2018

Safari inaendelea,

Layers

Oda ya Broiler inayoendelea kupokelewa sasa ni Tar 12/07/2018 ukiweka oda sasa utapokea tarehe 12 mwezi July.Ni vifarang...
20/06/2018

Oda ya Broiler inayoendelea kupokelewa sasa ni Tar 12/07/2018 ukiweka oda sasa utapokea tarehe 12 mwezi July.
Ni vifaranga vya Broiler bei ni Tshs. 1600/= kwa kifaranga,
tunauza kuanzia vifaranga 100 sawa na Box 1.

Ofisi ipo Ukonga,Dar Es Salaam,Tanzania

Moja ya mteja wetu aliyeweka oda ya vifaranga vya Broiler na Malawi akikamilisha banda lake maeneo ya Tabata Kifuru.Ufug...
19/06/2018

Moja ya mteja wetu aliyeweka oda ya vifaranga vya Broiler na Malawi akikamilisha banda lake maeneo ya Tabata Kifuru.

Ufugaji ni Kujali

Tunawatakia Watanzania wote Eid Mubarak,We wish all Tanzanians Eid Mubarak.
15/06/2018

Tunawatakia Watanzania wote Eid Mubarak,

We wish all Tanzanians Eid Mubarak.

07/06/2018

za wakati huu mfugaji,
Tar 10 baadhi ya staff wetu watakuwa Dodoma na Tar 20 pia tutakuwa Iringa.
wafugaji wa mikoa hiyo tutapenda kukutana nanyi maana kukutana nanyi ni sehemu ya jukumu letu.
karibuni sana na asanteni kwa wakazi wa Dodoma na Iringa kwa kuitika kuwa wateja wetu wa vifaranga vya Broiler.

tunazidi kuwa
tunakutakia ushindi kwa siku ya leo

Je, wajua??   Mwezi June,July,August,September, October na November kuku wa nyama watakuwa wanahitajika sana sokoni??   ...
29/05/2018

Je, wajua??
Mwezi June,July,August,September, October na November kuku wa nyama watakuwa wanahitajika sana sokoni??
Usisubiri hadi wakati huo ufike ndio uanze kutafuta vifaranga vya Broiler, karibu HeCo Poultry Farm tukuhudumie.

Tupo Ukonga, Dar Es Salaam, Tanzania
Simu #: 0655338533 au 0754927820

26/05/2018

Bado tunaendelea kupokea oda ya Broiler kwa sasa oda zilizobaki ni za tar;

- Tar 10/06/2018 (zimebaki oda ya vifaranga 600)
- Tar 20/06/2018
- Tar 12/07/2018
- Tar 2/207/2018.

Wahi kuweka oda maana uhitaji ni mwingi.
Bei ya kifaranga cha Broiler ni 1600/=
Tunauza kuanzia vifaranga 100/box 1.

Tupo Ukonga, Dar Es Salaam, Tanzania
Nyote mnakaribishwa HeCo Poultry Farm

Address

Ukonga Moshi Bar
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 12:00
Wednesday 09:00 - 18:00
Thursday 09:00 - 18:00
Friday 09:00 - 18:00
Saturday 09:00 - 15:00

Telephone

+255655338533

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when HeCo Poultry Farm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to HeCo Poultry Farm:

Videos

Share

Category

Nearby pet stores & pet services


Other Urban Farms in Dar es Salaam

Show All